Showing posts with label SIMULIZI. Show all posts
Showing posts with label SIMULIZI. Show all posts

Tuesday, 20 October 2015

STORI YENYE MAFUNDISHO MAKUBWA

JARIBU KUSOMA STORI HII MPAKA MWISHO NA UTAJIFUNZA KITU


“Nilipofika nyumbani usiku ule, mke wangu aliponitayarishia chakula, nilimshika mkono na kumwambia, Kuna kitu nataka nikwambie. Mke wangu alikaa chini na kula chakula kimya akiwa tayari kunisikiliza. Tena nikagundua macho yake yalionyesha anaumizwa. Nilishindwa hata namna ya kuanza kufumbua kinywa changu. Lakini ilibidi nimwambie ili ajue nilikuwa nikifikiri nini juu yake.
Nataka kukupa talaka. Nilianza kusema kwa utulivu. Alionekana kutokereka na maneno yangu badala yake aliniuliza kwa sauti ya upole ‘kwa nini?’ Sikumjibu swali lake. Kutojibu kulimfanya akasirike. Akatupa kijiko na akanikaripia, ‘wewe si mwanamume!’ Usiku ule,hakukuwa na maongezi kati yetu. Alikuwa akilia kwa kwikwi. Nilifahamu kwamba alitaka kujua ni nini kimetokea kwenye ndoa yetu. Lakini kwa hakika nisingeweza kumpa jibu wala sababu ya kuridhisha; alionekana si mali kitu kwangu penzi langu lilihamia kwa Mary. Sikumpenda tena mke wangu mawazo yote yalikuwa kwa Mary. Kwa kweli nilimdharau mke wangu!
Huku moyo wangu ukijua wazi kwamba nafanya kosa, niliandika talaka ambayo ilionyesha kwamba yeye (mke wangu) angepata nyumba yetu, gari na atakuwa na hisa 30% ya kampuni yetu. Aliangalia talaka ile na kuichana vipande vipande.

Thursday, 7 May 2015

SIMULIZI YA MAISHA YA IRENE UWOYA

Kama Alivyosema, Irene  Uwoya Ameanza  Hivi Kuyanika Maisha Yake

  Kutoka kwenye ukursa wake mtandaoni,staa mrembo Irene Uwoya ameanza hivi;
Naitwa Irene pankras uwoya...ni mtoto wakwanza katika familia ya mzeee uwoya yenye watoto 2 na mdogo wangu wakuite aitwae babu!!!nimezaliwa dodoma hospital nimeishi dodoma nikasoma shule ya msimgi mlimwa la kwanza mpaka la tatu...Wazaz wangu 

Tuesday, 30 July 2013

NILITEKWA NA MAHARAMIA KWA MIEZI SITA

Judith na David Tebbut walikuwa likizo nchini Kenya wakati waliposhambuliwa na kundi la watu wenye silaha. David aliuawa na Judith alichukuliwa hadi Somalia ambako alishikiliwa mateka kwa miezi sita.
Ni baada ya mwaka mmoja tangu aachiliwe huru, anasimulia dhamira ya ajabu ya kusalimika mikononi mwa watekaji wake.


Alidhamiria kusalimika, na hilo ndilo lililomsukuma kuandika kitabu kuhusu maisha yake akiwa mateka, Safari Ndefu Nyumbani, na pia kuzungumza na BBC katika moja ya mahojiano nadra kuhusu mkasa huo.Unapokutana na Judith Tebbut – yeye anapenda kuitwa Jude – na utajiuliza kwanini, baada ya miezi sita ndani ya chumba kichafu, kilichojaa vitu, akila chakula cha mgao cha viazi na mchele, akidhihakiwa, kudhalilishwa na mara kwa mara akitishiwa kuuawa, anaonekana hakuumizwa na mvumilivu.

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...