JARIBU KUSOMA STORI HII MPAKA MWISHO NA UTAJIFUNZA KITU
“Nilipofika
nyumbani usiku ule, mke wangu aliponitayarishia chakula, nilimshika mkono na kumwambia,
Kuna kitu nataka nikwambie. Mke wangu alikaa chini na kula chakula kimya akiwa
tayari kunisikiliza. Tena nikagundua macho yake yalionyesha anaumizwa.
Nilishindwa hata namna ya kuanza kufumbua kinywa changu. Lakini ilibidi
nimwambie ili ajue nilikuwa nikifikiri nini juu yake.
Nataka
kukupa talaka. Nilianza kusema kwa utulivu. Alionekana kutokereka na maneno
yangu badala yake aliniuliza kwa sauti ya upole ‘kwa nini?’ Sikumjibu swali lake.
Kutojibu kulimfanya akasirike. Akatupa kijiko na akanikaripia, ‘wewe si
mwanamume!’ Usiku ule,hakukuwa na maongezi kati yetu. Alikuwa akilia kwa kwikwi.
Nilifahamu kwamba alitaka kujua ni nini kimetokea kwenye ndoa yetu. Lakini kwa
hakika nisingeweza kumpa jibu wala sababu ya kuridhisha; alionekana si mali
kitu kwangu penzi langu lilihamia kwa Mary. Sikumpenda tena mke wangu mawazo
yote yalikuwa kwa Mary. Kwa kweli nilimdharau mke
wangu!
Huku
moyo wangu ukijua wazi kwamba nafanya kosa, niliandika talaka ambayo ilionyesha
kwamba yeye (mke wangu) angepata nyumba yetu, gari na atakuwa na hisa 30% ya
kampuni yetu. Aliangalia talaka ile na kuichana vipande vipande.